ALIYEZUSHA HABARI ZA UONGO KWA MKUU WA MAJESHI GEN, MWAMUNYANGE AFIKISHWA MAHAKAMANI


Serikali leo imemfikisha mahakamani bwana Bernedict Ngonyani kwa tuhuma za kutumia mtandao wa facebook na whatsup kueneza taarifa za uongo kuwa mkuu wa majeshi ya Ulinzi Jenerali Davis Mwamunyange amelazwa Nairobi kwa madai ya kulishwa chakula chenye sumu.

Akizungumza kwenye eneo la mahakama ya kisutu jijini dar es salaam ambako mtuhumiwa huyo alifikishwa kwa ajili ya kusomewa mashtaka, wakili mkuu wa serikali Joanes Karungura amesema, mtuhumiwa huyo amefikishwa mahakamani hapo kwa kuvunja kifungu namba 16 cha sheria ya makosa ya kimtandao ya mwaka 2015.

Sheria hiyo ijulikanyo kwa lugha ya kiingereza CYBERCRIME inakataza kusambaza ujumbe, taarifa au data, za uongo au zisizothibitishwa kwa njia ya mtandao.

Usipitwe..Jiunge nami kupitia Facebook ,Twitter , Instagram , Youtube, kwa jina la +Sangu Joseph  and +255712861292 kwa matangazo





Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment