MSANII WA NYIMBO ZA INJILI WA SOUTH AFRICA #SOLLY MAHLANGU KUTUMBUIZA TAMASHA LA AMANI TANZANIA #OCT04

 
Mwimbaji wa kimataifa wa nyimbo za injili kutoka nchini Afrika Kusini Solly Mahlangu,amethibitisha kutumbuiza katika tamasha la kuombe amani  linalotarajiwa kufanyika Oktoba 4 katika uwanja wa Taifa Dar Es Salaam.

Mwenyekiti wa Tamasha hilo kutoka kampuni ya Msama Promotion,Alex Msama,amewaambia hayo waandishi wa habari jijini Dar Es Salaam  alipokuwa akizungumzia maendeleo ya maandalizi ya tamasha hilo sambamba na kutaja majina ya waimbaji wa nyimbo za injili wa ndani na nje ya nchi,watakao tumbuiza Oktoba 25 katika tamasha la kuombea amani

Msama,amesema,Maandalizi ya tamasha hilo yanaendelea vizuri ambapo kwa mara nyingine,ameeendelea kutaja majina ya waimbaji waliokwisha kuthibitisha kutumbuiza katika tamasha hilo,ambapo mbali  na Solly Mahlangu,amelitaja kundi la  Kelechi kutoka   nchini Uingereza kuwa  limethibitisha kuja kutumbuiza katika tamasha hilo.





Usipitwe..Jiunge nami kupitia Facebook ,Twitter , Instagram , Youtube, kwa jina la +Sangu Joseph  and +255712861292 kwa matangazo

Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment